Kwa matangazo ya video na Picha .. 📱 Tupigie simu 0742100740 📧 Email Shafiishayani@gmail.com WhatsApp 0689079948

Wednesday 12 July 2023

Baraza la Sanaa Zanzibar: Wanaume Wanaosukwa kama Wanawake kukamatwa, faini ni Tsh. Milioni 1 au kifungo cha Miezi 6

 Member

1689135807959.png
Serikali ya Mapinduzi Zanzibar imepiga marufuku tabia ya wanaume kusuka nywele na anayekamatwa faini yake ni Sh1 milioni au kifungu cha miezi sita au vyote kwa pamoja.

Akizungumza na Mwananchi leo Jumanne, Julai 11, 2023, Katibu Mtendaji Baraza la Sanaa, Sensa ya Elimu na Utamaduni Zanzibar, Dk Omar Adam amesema hatua hiyo inalenga kulinda silika na tamaduni za Kizanzibari.

Amesema katazo hilo ni kwa mujibu wa sheria namba saba ya mwaka 2015 inayolenga kulinda utamaduni, mila na desturi za Mzanzibari bila kuathiri mambo mengine.

“Zanzibar hairuhusu mwanaume kusuka nywele faini ya kusuka nywele kwa Zanzibar ni Sh1 milioni au miezi sita jela au vyote kwa pamoja,” amesema.

Amesema hakuna kibali wala kulipia ili uruhusiwe kusuka nywele kwa mwanamme kama ambavyo awali ilisambaa kwennye mitandao ya kijamii.

“Sheria ilikuwa haijaanza kutekelezwa kwa kutoa faini lakini imeshatokea kama mara tatu mtu anakamatwa na kupewa onyo na wengine wapo wamejirekebisha na wengine wanaendelea kujirekebisha,” amesema

Hata hivyo, amesema katazo hilo haliwahusu Wamaasai kwasababu wanatambua kwamba huo ndio utamaduni wao kwamba mwanaume anasuka na mwanamke ananyoa au naye anasuka.

Kuhusu suala la kuathiri utalii wa Zanzibar, Katibu huyo amesema haliwezi kuathiri kwa sababu utafiti alioufanya kwanza watalii wengi hawasuki huo ni utamaduni ambao umetokea huku.

Kuhusu wasanii, amesema iwapo kuna msanii anataka kufanya shughuli zake wanaweza kukutana naye wakazungumza akavaa kofia mpaka anapokwenda kwenye maonyesho yake.

“Tunachosema suala la ushirikiano wa Muungano kisiwei kichaka cha kuharibu tamaduni silka na atamaduni za Kizanzibar ni akam ilivyo bangi hatuwezi kuruhusu kwamba ziendeel huku asili tuliochiwa na wazee wetu inapotea na katika sula hili tumejipanga tutakuwa wakali sana” alisema

Amesema watapitia hata kwenye shule kutoa elimu hiyo kwa walimu na wanafunzi ili kuwadhibiti wnafunzi wenye tabia hizo.

Sio mara ya kwanza kwa Zanzibar kutoa makatazo kama hayo, mwaka 2021 aliyekuwa Waziri wa Utalii na Mambo ya Kale, Lela Musa alipiga marufuku kuvaa nguo fupi (nusu uchi) kwa watalii ili kulinda utamaduni wa Zanzibar

Agizo hilo lilitolewa, huku ikielezwa iwapo wakibainika wameevaa nguo zisizo na stara atakamatwa anayewatembeza na kutozwa faini, hata hivyo jambo hilo utekelzaji wake haukuzingatiwa.

Pia, Mkuu wa Wilaya ya Mjini, Rashidi Msaraka aliwahi kupiga marufuku vijana wanaonyoa viduku ambapo aliwahi kuwakamata na kuchukua mkasi kuwanyoa, hata hivyo nalo halikuwa na mwendelezo wake.

No comments:

Post a Comment

MIUNDOMBINU YA SHULE YA MSINGI MAGOMENI.

Wiki mbili baada ya mwandishi wa habari wa Gazeti la Nipashe kuzungumza na uongozi wa Wilaya ya Tunduru kutaka kujua kwanini Shule ya Msingi...