Kwa matangazo ya video na Picha .. 📱 Tupigie simu 0742100740 📧 Email Shafiishayani@gmail.com WhatsApp 0689079948

Sunday 16 July 2023

AWE yawapatia mafunzo wanawake kuwa Wajasriamali bora Afrika Mashariki

 Naye balozi wa Marekani nchini Tanzania Michael Battle alisema kuna umuhimu mkubwa kwa wajasriamali wanawake kukutana na kupeana elimu juu ya masuala ya kijasiriamali ili kumaliza umasikini katika ukanda huo ya wa Afrika mashariki.

Balozi wa Marekani nchini Tanzania Michael Battle.
Balozi wa Marekani nchini Tanzania Michael Battle.

Balozi huyo wa Marekani alisema,“ni muhimu kwa wanawake wajasiriamali kupata nafasi ya kuungana kwa pamoja na njia pekee ya kumaliza umaskini katika Afrika Mashariki ni kuwa na wanawake wenye nguvu sana ambao wanajihusisha na biashara zinazoungwa mkono na taifa lao na kuungwa mkono na wanaume wa taifa lao pia hii inaleta tofauti katika kupanda kwa mtu binafsi na inafanya tofauti katika kukua kwa taifa.”

Hata hivyo mkufunzi na mjasiriamali Victoria kisyombe, alimalizia kwa kusisitiza nchi za Afrika kutambua umuhimu wa mwanamke kushiriki katika shughuli za maendeleo ya kiuchumi kwani kumuendeleza mwanamke ni kuendeleza familia, jamii na taifa kwa ujumla.

Imetayaraishwa na Amri Ramadhani Sauti ya Amerika, Dar es salaam.

No comments:

Post a Comment

MIUNDOMBINU YA SHULE YA MSINGI MAGOMENI.

Wiki mbili baada ya mwandishi wa habari wa Gazeti la Nipashe kuzungumza na uongozi wa Wilaya ya Tunduru kutaka kujua kwanini Shule ya Msingi...